Sunday, 6 March 2016

Leo tarehe, 27 /02 /2015 Asasi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania (AWAMATA)  ikishirikiana na Friends of Fatema pamoja na Mtanzania Jitambue (MJ). Tumetoa Msaada wa kufanya FUMIGATION kwenye mabweni manne  katika WATOTO wenye ULEMAVU wa Ngozi Kambi ya BUHANGIJA SHINYANGA mjini. Hivyo basi kutokana na mchango nilioomba kuchangisha kwa radhaa za maadimin  ili kuwasaidia watoto hao wenye mazingira magumu, jumla ya pesa taslimu  Tsh.305,000/= zilipatikana na kiasi cha  Tsh.190,000/= ndio kilichotumika kwa FUMIGATION  hiyo. Aidha kiasi cha Tshs.110,000/= kilichobaki kimetumika kufanya maintanance ya miundo mbinu ya maji kambini hapo ambapo walikua wanakosa maji safi na salama ya bomba kwa ubovu wa koki 4  za maji pia  Mabweni 2 yalikua hayana umeme na fundi amaendelea na kutengeneza.  sambamba na hilo pesa kidogo iliyo baki imetumika kununua catton ya sabuni za kufulia na sukari kilo 5.

Sambamba na hayo pia nimekabidhi nguo za watoto wa kike  pieces 86 na  nguo za kiume pieces 18 ambazo zilitumwa na Dk.Shaban(Aluta) kwa niaba ya Friends of Fatema.
Haya yote yamekwenda sambamba na kufanya usafi  katika Kambi hiyo kama agizo la Rais linavyoelekeza kila jumamosi ya mwisho wa mwezi.  

Kwa niaba ya  WATOTO napenda kutoashukrani za dhati kabisa  kwa wakioguswa na ombi langu kwani chamgamoto ya kunguni  kwao limetatuliwa kutokana na mchango wetu wa hiari.

Mpatapo nafasi mfike kambini mjionee.

ASANTENI SANA
Ndg.Andrew Malulu
Kwa niaba ya Asasi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania, Friends of Fatema na Mtanzania Jitambue

Powered by Blogger.

Popular Posts

Recent Posts

Recent Posts Widget

Fellow Bloggers